Upatikanaji wa bima ya maisha, hospitali na ajali imerahisishwa. Bima Mkononi inawawezesha wateja wa Tigo kujiunga na bima kiurahisi na kwa karaka kwa kupitia simu zao. Ukijiunga, furahia gharama moja pekee tu kwa watu wote walio kati ya umri wa miaka 18 - 65. Kujiunga inachukua dakika chache tu na unaweza kulipa kwa kupitia Tigo Pesa au kwa kulipa pesa taslimu kwenye kituo chochote cha Tigo huduma kwa wateja.
Jinsi ya kujiunga na Bima Mkononi
1. Chagua bima unayohitaji, gharama na muda wa kudumu kati ya hizo zilizoorodheshwa hapo chini.
2. Piga #148*15# na ufuate maelekezo
Aina za bima na gharama kutoka Bima Mkononi
Aina ya Bima | Manufaa | Gharama (TZS) | Muda wa Kudumu |
Bima ya kulazwa |
Pata fidia ya TZS 40,000 kwa siku - Unaruhusiwa kulazwa kwa sku 30 na kwa gharama isiyo zidi TZS 1,000,000 | 2,999 | Miezi 2 |
7,999 | Miezi 6 | ||
15,999 | Miezi 13 | ||
Bima ya maisha |
Mwenye bima hii atapata TZS 1,000,000. Walengwa watapata TZS 500,000 ikiwa kwamba mwenye bima ndio mlengwa. |
2,999 | Miezi 2 |
7,999 | Miezi 6 | ||
15,999 | Miezi 13 | ||
Bima ya ajali |
Kwa kutegemea na ulemavu au kifo, pata hadi TZS 3,000,000 | 1,999 | Miezi 2 |
4,999 | Miezi 6 | ||
9,999 | Miezi 13 |